Kweli hakuna anayefurahia kuachwa. Mapenzi
yanauma, wakati mwingine hasira zinaweza kutuongoza katika kufanya maamuzi
lakini suala la msingi linalopaswa kuzingatia ni kujidhibiti. Lazima tujifunze
kudhibiti hasira zetu.
Kuachwa au kuachana siyo mwisho wa maisha.
Kweli mnaweza kuwa mmewekeza nguvu, ndugu na hata marafiki katika uhusiano wenu
lakini endapo imetokea mmeshindwa kuendelea na safari kwa namna moja au
nyingine basi hakuna budi kushukuru na kuliacha lipite.
Usimuone mwenzako kama adui bali chukulia
kama changamoto katika maisha yako kwani hujui pengine ni nini kingetokea kama
ungeendelea na safari hiyo. Yawezekana Mungu amekuepusha na jambo lingine zito
huko mbeleni.
Mshukuru yeye, usiwachukie marafiki,
usiwakasirikie ndugu zake wala yeye mwenyewe. Mchukulie kama tu alikuwa mpenzi
wako. Mheshimu maana pia anazo siri zako nyingi. Anakujua vizuri hivyo kama
itakupendeza pia muombee mafanikio.
Muombe naye akuombee pia wewe katika safari
yako. Kama una shida ambayo unaona yeye anaweza kuwa msaada kwako, mueleze.
Kama atakuwa ni muungwana anaweza kukusaidia. Zungumza na marafiki na ndugu
zake kama vile hakuna kitu chochote kilichotokea.
Yawezekana hili likakushinda katika kipindi
cha awali lakini jipe moyo. Baadaye utaweza. Msalimie ukimuona barabarani. Hii
inakufanya uonekane mstaarabu hata kwa ndugu zake hivyo itakuwa jambo jema pia
kwao hata kuweza pia kufufua upya penzi lenu.
Kuna fursa ambazo anaweza kukupa au wewe
ukampa hata kama mmetengana. Weka uhusiano pembeni, ruhusu moyo wako uwe katika
hali ya urafiki. Urafiki utakupa fursa nyingi na endapo yeye au wewe utampata
mwenza basi mtaambizana.
Kila mmoja atakuwa huru na hapo kidogo
mawasiliano yanaweza kupungua ili kuepuka migogoro na wenza wenu wapya lakini
inapowezekana mnaweza kusalimiana. Hayo ndiyo maisha na hakuna sababu ya
kuwekeana chuki katika dunia hii iliyojaa nafasi nyingi maishani.
EmoticonEmoticon