Tatizo la
ugumba limekua kubwa na umefika wakati lizungumzwe kwa kuangalia upande wa pili
wa shilingi.
Inaelezwa kuwa katika kila ndoa sita, moja
huhangaika kupata uzazi na mmoja kati ya wawili hao anaweza kuwa mgumba.
Zipo sababu mbalimbali zinazochangia ugumba
kwa wanaume ikiwamo matatizo ya kuzaliwa nayo au kuyapata ukubwani ikiwemo
magonjwa mbalimbali.
Matatizo yafuatayo yamekuwa ndiyo mara kwa mara chanzo cha
kujitokeza kwa tatizo la ugumba kwa wanaume.
Yako mambo yanayosababisha
utengenezaji wa mbegu zisizo na ubora zinazokosa ufanisi wa kazi yake. Mambo
hayo ni pamoja na kuzaliwa na korodani ambazo hazijashuka kutoka tumboni.
Kwa kawaida, kabla ya kuzaliwa kokwa za kiume
huwa zipo ndani ya pango la tumbo na hutakiwa zishuke kuelekea sehemu za uzazi
baada ya kuzaliwa.
Kushindwa kushuka na kuhifadhiwa katika korodani husababisha
mbegu au kokwa kuharibika kutokana na joto kali la tumboni.
Kushuka na
kuning’inia kwa korodani ni maumbile sahihi ya kibailojia yenye tija kiafya
ambayo huwezesha kupata joto la wastani hivyo kutengenezwa mbegu zenye kiwango.
Matatizo kwenye mfumo wa chembe za urithi.
Mwanadamu anaweza kurithi chembe za urithi zenye maelekezo ya kimwili yasiyo ya
kwaida hivyo kujikuta akizalisha mbegu zisizo na ubora.
Maambukizi ya virusi
hatari ikiwamo virusi vya mumps na maambukizi sugu ya magonjwa maeneo ya uzazi,
huchangia ugumba kwa mwanaume.
Ajali za bahati mbaya zinazotokea wakati wa
upasuaji wa kurekebisha matatizo ya kiafya ikiwemo katika korodani au ngiri
(hernia) na aina ya kizamani ya upasuaji wa tezi dume. Hili pia huchangia
tatizo la ugumba kwa wanaume.
Kuwahi kuasiliwa na kufungwa kitanzi katika mrija
kama njia za uzazi wa mpango husababisha ugumba.
Kuongezeka ukubwa wa mishipa inayorudisha
damu mwilini kutoka katika korodani au kokwa huweza kusababisha damu kwenda kwa
kasi eneo hilo na kuongeza joto hivyo kuathiri ufanisi wa utengenezaji wa mbegu
hizo ikiwemo wingi wake na maumbile.
Uwepo wa vizuizi katika utolewaji wa mbegu za
kiume huweza kuwa na tatizo.
Matatizo ya kujamiiana ikiwemo wanaume kuwa na
tatizo la kutoa mbegu haraka isivyo kawaida wakati wa tendo.
Tatizo la mbegu
kuchepukia katika kibofu cha mkojo badala ya kupitia katika mrija wa mkojo,
huwa ni sababu mojawapo ya ugumba.
Kuugua magonjwa ya zinaa hadi kufikia madhara
ya kuharibu mfumo mzima wa utengenezwaji wa mbegu za kiume, huangukia katika
tatizo hili.
Zipo baadhi ya kemikali ambazo kama mwanaume zitamwingia mwilini
au kukaa katika maeneo yenye kemikali hizo kwa muda mrefu, zinaweza kumletea
ugumba.
Kemikali hizo ni kama madawa ya kilimo, rangi, mipira, mionzi na dawa
za steriods.
Unywaji pombe kupindukia ni tatizo ambalo
limekuwa likizidi kuwa kubwa.
Hii ni kutokana na maendeleo ya kichumi, watu
wengi wamejiingiza katika unywaji wa pombe uliopindukia. Matumizi ya madawa ya
kulevya kama cocaine, bangi, hashishi, mihadarati yote hayo hupunguza idadi na
kiwango cha mbegu za kiume (sperms).
Madhara ya saratani na matibabu yake ambayo
yanahusisha mionzi na kemikali tiba za saratani nazo zinaweza kuathiri
utengenezwaji wa mbegu za kiume.
Uondolewaji wa kokwa za kiume baada ya kupata
saratani au uvimbe ni chanzo kingine cha ugumba au wengine wanaweza kupata
ajali maeneo ya uzazi na kuwafanya wagumba.
TIBA NA USHAURI
Yeyote ambaye ana matatizo tuliyoyaanisha
hapo juu anatakiwa kuonana na daktari ili apimwe na kama tatizo lake litahitaji
dawa atapatiwa, lakini pia anaweza kupewa ushauri ikiwa itagundulika kuwa ana
matatizo hayo.
EmoticonEmoticon