1.Je, mwanamke anaweza kufikia mshindo?
Ndiyo, mwanamke anaweza kufikia mshindo wakati wa
kujamiiana. Dalili ya mwanamke kufikia mshindo katika kujamiiana ni ile hali ya
pekee ya kujisikia vizuri kimwili. Tofauti na mwanaume, anapofikia mshindo
mwanamke hakojoi kitu chochote.
Kwa kawaida mwanaume anakojoa manii wakati wa kujamii ana
anapofikia mshindo. Kwa sababu dalili hii ni rahisi kuona baadhi ya watu
wanadhani kwamba ni wanaume tu wanaofikia mshindo wakati wa kujamii ana. Lakini
hii siyo kweli. Mwanamke pia hufikia mshindo, ingawa siyo rahisi kuuona.
2.Je, kwa nini mwanamke akigongwa na uume kwenye uke yaani juu hutoa
majimaji kupitia ukeni?
Kugusana kwa kutumia viungo vya uzazi ni njia mojawapo ya kuamsha
hisia ya kujamii ana. Kama mwanamke anatoa majimaji baada ya kugusana na uume
kwenye uke, ina maana kwamba ameshikwa na ashiki kubwa.
Majimaji hayo
yanarahisisha uume kupenya ukeni. Chanzo cha majimaji hayo ni vifuko maalumu
vilivyomo ndani ya uke.
3.Njia zipi
zinaweza kumletea mwanamke mshindo haraka, na zipi zinamletea mwanaume mshindo
haraka?
Jambo la msingi kabisa ni kwamba wote wawili kuwa tayari kwa
kujamii ana. Yaani kupendana na kujaliana sana, halafu kuwa tayari kwa tendo
hilo kimwili, kimawazo na kiakili. Kutokuwa tayari kwa kufanya mapenzi, kwa
mfano kwa sababu ya kuogopa ujauzito, inamzuia mtu yeyote kufikia mshindo.
Kama wote wawili mpo tayari, kufikia mshindo au kutofikia kunategemea maandalizi ya awali ya mapenzi.
Mnatakiwa kukubaliana jinsi mtakavyofanya mapenzi i i ili kila mmoja wenu aweze kufurahia na kuridhika.
Kwa uhakika, kila mwanamke na mwanaume anazo sehemu
maalumu ambazo ukigusa basi ni rahisi sana kufikia mshindo. Upeo wa hali ya kujamiiana pia unaweza kufikia kwa kupiga punyeto.
Kwa mfano,
mwanaume anaweza kugusa uume wake au mwanamke anaweza kusugua taratibu kinembe
mpaka anafikia mshindo. Kupiga punyeto ni njia i iliyo salama ya kumaliza hamu
ya kutaka kufanya mapenzi na haina athari mbaya kiafya.
4.Kwa nini mara nyingi mvulana ni mwepesi sana katika kuanzisha kufanya
mapenzi? Na kwa nini mwanaume mara nyingi anafikia mshindo kabla ya mwanamke?
Kwa kawaida i inakubalika kuwa wavulana ndiyo waaanze kuonyesha
ishara za kujamiaana na tafiti zimeonyesha kwamba mara nyingi mwanaume anafikia
mshindo kabla ya mwanamke. Hii ni ukweli katika sehemu nyingi za dunia.
Baadhi ya wavulana wanatumia vibaya uwezo wao wa kufanya mapenzi. Wanafuatafuata wasichana na kuwatongoza i ili wafanye mapenzi katika umri mdogo. Hata hivyo kujamii ana katika umri mdogo kunaweza kusababisha athari nyingi kama vile mimba isiyotarajiwa au kuambukizwa magonjwa ya zinaa.
Kwa
hiyo, wavulana wanashauriwa kuwa wavumilivu licha ya mivuto hiyo ya kutaka
kujamii ana, kwa sababu kwa njia ya kujamii ana ovyo mnahatarisha maisha yenu
ya baadaye. Kuna njia nyingine za kuonyesha mapenzi, kama vile kubusu,
kukumbatia, kushikana mikono na hata kupiga punyeto.
Kimaumbile, mara nyingi mwanaume anafikia mshindo haraka zaidi kuliko mwanamke.
Lakini, mkihakikisha kwamba mwanamke ni tayari kwa kujamiiana na kama
mmechukua muda wa kutosha kujiaanda vizuri, mnaweza kufikia mshindo pamoja.
Hivyo kuwaletea raha na starehe wote wawili.
EmoticonEmoticon