
Kuna wengi wanaojipata katika hali ya kutisha
ya ndoa zao kufa wakiwa bado ndani. Kuna mambo ambayo yanafaa kuendelea katika
ndoa yako lakini kila kitu kimesimama.
Hizi hapa dalili kwamba upo katika ndoa
‘iliyokufa’ na unafaa kuanza kuchukua hatua za kuifufua au kuamua kufunga
virago na kuondoka.
1. Hakuna tendo la ndoa
Endapo kuna sababu za
kimatibabu kutoshiriki tendo la ndoa na mwenzako, basi itaeleweka lakini iwapo
kila kitu kipo sawa lakini nyote au mmoja wenu hana hamu na mwenzake basi
dalili hii ni mbaya kwa maisha ya ndoa yenu.
2. Huna cha kumuambia mwenzake
Iwapo kuna jambo linalokufanyikia kazini au umesajili
mafanikio fulani na mwenzako sio miongoni mwa watu wa kwanza kujuzwa, basi
kwisha mambo. Humuoni kama mtu muhimu katika maisha yako anayefaa kufahamu yote
yanayofanyika katika maisha yako. Endapo utapata ugumu wa kufanya gumzo za hapa
na pale na mwenzako katika ndoa, basi umefika mwisho na umechoka.
3. Mko pamoja lakini sio pamoja
Endapo mtajipata katika nyumba moja na kila mtu
anajishughulisha na mambo yake bila utangamano wa pamoja basi mko pamoja kwa
njia tofauti. Hatua hiyo humaanisha kwamba hakuna tena kinachowaunganisha kwa
dhamira moja.
4.Unajishughulisha
na mambo na matatizo ya watu wengine
Wanawake wana mazoea ya kujishughulisha na matatizo ya
watu wengine ili kuficha machungu wanayopitia. Endapo utajipata unajiingiza
sana katika masuala ya wengine basi dalili hiyo ni ya kwamba unajaribu
kujishughulisha ujipe muda mbali na masaibu yako.
5. Pengo kati yenu linazidi kupanuka
Endapo utajipata kwamba kila
wakati mnapozungumza malumbano yanazuka na kuwatenganisha zaidi, basi
dalili hiyo sio nzuri. Ni kawaida kwa wanandoa kupitia nyakati ngumu lakini
zikianza kudumu kwa muda mrefu basi zitakuwa mtindo wa kila siku na kuvuruga
ndoa yenu.
6. Unaanza kutamani maisha bila mwenzako
Iwapo utawahi kufikiria
kuhusu uwezo wako kuwa na furaha bila mwenzako maishani mwako, basi hilo sio
jambo zuri. Hiyo ni mojawapo ya hatua za kujiondoa kihisia kutoka kwake na ni
dalili kwamba mambo kati yeni yamevurugika kwa kiwango kikubwa.
7.
Mmeacha kupigana
Endapo mtakoma kupigana au
malumbano kwa kusalimu amri, ni ishara kwamba mmefika mwisho wa safari yenu ya
ndoa. Anachofanya mwenzako hakikwazi na hivyo basi hujali kuhusu maamuzi au
mkondo anaochukua.
8. Unahisi kwamba hakusikizi
Endapo mmoja wenu atahisi
kana kwamba mwenzake hampi muda wa kumsikiza au kuzingatia mchango wake katika
ndoa basi dalili hiyo ni mbaya kwa ndoa yenu. Njia bora ya kusuluhisha mizozo
katika ndoa sio tu kuelewa tatizo bali pia kusikiliza kuanzia mwanzo.
9. Unawatembelea marafiki zako
badala ya mwenzako
Unapojipata unatafita sababu
za kuwatembelea rafiki zako badala ya mume au mkeo basi fahamu kwamba mambo
yamevuka mipaka. Endapo kumuona mwenzako kunazua makovu na hamaki ya matatizo
ambayo hamkuyasuluhisha ni daalili kwamba mnafaa kuanza kutafuta njia za
kujikwamua kutoka hali hiyo.
10. Hamna muda pamoja
Unapofika nyumbani baada ya
siku ndefu ya kazi na uchovu, mnakaa pamoja sebuleni au kila mtu anaendelea na
shughuli zake? Endapo hakuna aliye na muda na mwenzake, dalili hiyo sio nzuri
kwa ndoa yenu.
11. Hayupo katika orodha ya vipaumbele
Wapendanao hujali sana
kuhusu wenzao katika ndoa na iwapo utajipata huna muda hata wa kumfikiria au
kujali kuhusu anachofanya, basi fahamu kwamba kuna tatizo na ndoa yenu ipo
katika hatua mbaya.
12. Mwenzao hayuko tayari kufanya juhudi za
kuboresha ndoa yenu
Endapo umejipata katika kibarua cha kuikwamua ndoa yenu
peke yako na mwenzio hana mbio, basi jua kwamba ndoa hiyo imefika tamati.
EmoticonEmoticon