Mara nyingi tumeshuhudia katika
familia nyingi mwanaume akitangulia kufa kabla ya mwanamke. Simaanishi kuwa
wanaume wote wanakufa mapema, lakini mara nyingi wanawake huishi zaidi kuliko
wanaume.
Utafiti zaidi juu ya sababu za
wanaume wengi kufa mapema kuliko wanawake.
1. Wanawake hujali afya zao
zaidi
Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya zilibaini kuwa wanawake hujali afya zao zaidi. Tafiti hizo zinaeleza kuwa wanawake wengi wanapojihisi kuumwa huenda hosipitalini ili kupata ushauri wa kitaalamu.
Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya zilibaini kuwa wanawake hujali afya zao zaidi. Tafiti hizo zinaeleza kuwa wanawake wengi wanapojihisi kuumwa huenda hosipitalini ili kupata ushauri wa kitaalamu.
2. Wanaume huendeleza tabia
hatarishi zaidi
Tabia kama vile uvutaji wa sigara, pombe au madawa ya kulevya mara nyingi hufanywa na wanaume. Hili limepelekea kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa na kusababisha kufupisha maisha ya wanaume wengi.
Tabia kama vile uvutaji wa sigara, pombe au madawa ya kulevya mara nyingi hufanywa na wanaume. Hili limepelekea kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa na kusababisha kufupisha maisha ya wanaume wengi.
3. Wanaume hujiua zaidi
kuliko wanawake
Takwimu mbalimbali zinaonyesha kuwa kiwango cha vifo vinavyotokana na kujiua kwa wanaume ni kikubwa kuliko kwa wanawake.
Takwimu mbalimbali zinaonyesha kuwa kiwango cha vifo vinavyotokana na kujiua kwa wanaume ni kikubwa kuliko kwa wanawake.
4. Wanawake wanapenda
kushirikisha watu wengine
Kuna usemi usemao “mwanaume ana kifua cha kutunza mambo”; kwa hakika kwa upande mwingine hili ndilo huchangia wanaume kufa mapema.
Kuna usemi usemao “mwanaume ana kifua cha kutunza mambo”; kwa hakika kwa upande mwingine hili ndilo huchangia wanaume kufa mapema.
5. Maradhi ya moyo huchelewa
kutokea kwa wanawake
Tafiti zilizofanywa huko Marekani, zilibaini kuwa maradhi ya moyo huua wanaume na wanawake lakini maradhi haya huchelewa kwa takriban miaka 10 kwa mwanamke.
Tafiti zilizofanywa huko Marekani, zilibaini kuwa maradhi ya moyo huua wanaume na wanawake lakini maradhi haya huchelewa kwa takriban miaka 10 kwa mwanamke.
6. Kazi wanazofanya wanaume
zinawachakaza
Naamini swala la kazi ngumu au hatari kwa wanaume linafahamika wazi, wanaume hufanya shughuli za shuruba bila hata kupumzika au kula vyema.
Naamini swala la kazi ngumu au hatari kwa wanaume linafahamika wazi, wanaume hufanya shughuli za shuruba bila hata kupumzika au kula vyema.
Kwa hakika uhai wa mtu uko mikononi
mwa MUNGU, lakini kuna badhii ya mambo huchangia kufupisha uhai wa mtu. Ikiwa
wewe ni mwanaume na unaweza kuyaepuka badhii ya mambo yaliyoelezwa hapa, basi
fanya hivyo ili angalau uongeze siku kadhaa.
EmoticonEmoticon