Baada ya wengi kuanza kusema kwamba
huwenda bifu kati yao bado linaendelea, Nas ameizungumzia ishu ya Jay-Z kuachia
ngoma kila baada ya ujio wake.
Wiki hii Nas
ameachia album yake mpya "King's Disease" lakini siku kadhaa nyuma
kabla ya kuiachia, Jay-Z na Pharrell Williams waliachia mkwaju mpya
"Entrepreneur" ambapo wengi walikuja na kauli kwamba Jay amekuwa
akifanya hivyo mara kwa mara Nas akitaka kuachia kazi.
Sasa kwenye
mahojiano na The Breakfast Club, Nas amejibu kwa kusema hafikirii kama ni bifu kati
yao bali ni bahati mbaya tu wamekuwa wakigongana kwenye uachiaji kazi.
Kwenye mahojiano
hayo pia, Nas alijibu kwanini hakuwahi kufanya ngoma yoyote na The Notorious
B.I.G , alisema kuna siku walikuwa studio pamoja wakitaka kufanya ngoma kadhaa
ikiwemo remix ya "Gimme The Loot" lakini waliishia kuvuta bangi kwa
wingi kiasi cha kuwafanya kuwa "High" na walipokuja kuzinduka
walijikuta wamechoka sana kiasi cha kushindwa kufanya chochote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon