Tattoo ni uwekaji wa wino kwenye ngozi ya ndani kitaalamu kama
dermis kubadilisha rangi kabisa maisha yako yote au kwa muda tu, inateemea na
uwekaji..
Madhara Ya Tattoo
1. Kansa ya ngozi
Hapo mwanzoni wataalamu walikua wanasema hakuna mahusiano
kati ya kansa ya ngozi na na tabia ya kujichora tattoo lakini hivi karibuni
tafiti kutoka uingereza zinaonyesha kuna aina fulani za wino ambazo zinaweza
kusababisha kansa zikitumika kuchora tattoo.
2. Allergy ya Ngozi
2. Allergy ya Ngozi
Haijalishi unaweka tattoo kwa muda au ya moja kwa moja
kumetokea kesi nyingi za watu wanaopata allergy baada ya kupakwa tattoo,
utafiti unaonyesha rangi nyekundu ndio inaongoza kwa kusababisha allergy hizo
huku rangi zingine kama nyeusi, purple na zingine hazisababishi.
3. Makovu
3. Makovu
Mwili unataambua tattoo kama adui wake hivyo hujaribu
kuiondoa kwa njia mbalimbali na kwa kufanya hivyo husababisha makovu ya muda
mrefu ambayo yanaweza kuleta magonjwa mengine ya ngozi.
4. Maambukizi ya ukimwi na ugonjwa wa hepatitis
4. Maambukizi ya ukimwi na ugonjwa wa hepatitis
Tabia ya kurudia sindano zilezile wakati wa kuchora tattoo
kunaweza kusababisha maambukizi ya virusi vya ukimwi na maambukizi ya virusi
vinavyoshambulia ini kitaalamu kama hepatitis b.
5. Matatizo kipindi cha kufanya kipimo cha MRI
5. Matatizo kipindi cha kufanya kipimo cha MRI
Hichi kipimo ni cha mionzi na kirefu chake ni magnetic
resonance imaging, hutumika kupima viungo vya mwili ambavyo havionekani kwa
macho ndani ya mwili wa binadamu kama x ray inavyofanya.
6. Kubadilika kwa ngozi ya rangi
6. Kubadilika kwa ngozi ya rangi
Sehemu inayochorwa tattoo hubadilika moja kwa moja na kua na
rangi tofauti, hakuna jinsi unaweza ukaitoa hiyo rangi tena, hata baada ya muda
mrefu tattoo ikipungua nguvu lakini ngozi haiwezi kua kama zamani.
7. Hutaruhusiwa kuchangia damu
7. Hutaruhusiwa kuchangia damu
Mara nyingi watu wenye tattoo hawaruhusiwi kuchangia damu
kwani wana hatari ya kusambaza ugonjwa kwenda kwa mtu mwingine, kimsingi mtu
aliyechora ndani ya muda mfupi ndio haruhusiwi lakini kwasababu wakati mwingine
sio rahisi kutofautisha tattoo mpya na ya zamani basi hawa watu huwa
hawaruhusiwi kabisa.mchezaji wa kimataifa christian ronaldo hachori tattoo kwa
sababu ya hili.
8. Unaweza kukosa fursa mbalimbali
8. Unaweza kukosa fursa mbalimbali
Kuna kampuni mbalimbali duniani haziwapi watu kazi kwasababu
wamechora tattoo kulingana na imani za kampuni husika lakini pia kazi yeyote ya
jeshi duniani hairuhusu tattoo hivyo kama wewe unayesoma hapa umeshachora
tattoo ujue kazi ya jeshi huna tena.
9. Tattoo huingiliana na matumizi ya dawa Fulani
9. Tattoo huingiliana na matumizi ya dawa Fulani
Kama wewe unatumia dawa za kuzuia damu isingane mwilini
ukichora tattoo inaweza kufanya utoke damu nyingi sana kwani dawa hizo huzuia
uwezo wa mwili kukausha damu na kuponyesha vidonda.
10. Magonjwa ya Ngozi
10. Magonjwa ya Ngozi
Wakati mwingine bacteria huweza kuvamia sehemu zenye vidonda
vya tattoo na kusababisha kutopona haraka, dalili huweza kua homa kali, maunivu
makali na sehemu ya tattoo kuvimba.
11. Damu kuganda juu ya ngozi[haematoma]
11. Damu kuganda juu ya ngozi[haematoma]
Hii husababishwa na kuvuja kwa damu nyingi
chini ya ngozi, huonekana sana pembeni pembeni ya sehemu ambapo rangi ya tatoo
imepita na huchelewesha kupona kwa kidonda.
EmoticonEmoticon