Wafungwa waliorudi wamewaambia maafisa kwamba walilazimishwa
kutoroka na
wanapendelea kuendelea kukaa gerezani badala ya kuishi na waasi.
Wafungwa 20 kati ya 1,300 waliotoroka gerezani katika mji wa
Beni, mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wamerudi gerezani muda
mfupi baada ya kutoroka.
Wafungwa waliorudi wamewaambia maafisa kwamba wanapendelea
kuendelea kukaa gerezani badala ya kuishi na waasi.
Kulingana na Meya wa mji wa Beni Modeste Bakwanamaha,
wafungwa waliorudi wamesema kwamba “walichukuliwa kwa nguvu na kwamba
wamewatoroka waasi wa Allied Democratic Forces –ADF - waliowateka nyara baada
ya kuvunja gereza jumanne asubuhi.”
Watu waliokuwa wamejihami kwa bunduki, wanaoaminika kuwa
wapiganaji wa kundi la ADF walivamia gereza la Kangbayi, mjini Beni na
kuachilia huru zaidi ya wafungwa 1,300. Wafungwa 100 pekee walisalia gerezani.
Kulingana na Meya Bakwanamaha, “washambuliaji walikuwa wengi na walifanikiwa kuvunja milango ya gereza kwa kutumia machine za wahunzi zinazotumia umeme.”
EmoticonEmoticon