Bomu kubwa
ambalo halikulipuka katika vita ya pili ya dunia lililobainika nchini Poland
limelipuka wakati wa shughuli ya kulitegua, msemaji wa jeshi la wanamaji nchini
humo ameeleza.
Uwezekano
wa bomu hilo lililokuwa chini ya bahari kulipuka ulikuwa ukitarajiwa na wapiga
mbizi wote waliohusika kwenye tukio hilo hawakujeruhiwa.
Karibu
wakazi 750 waliondolewa karibu na mji wa bandari wa Swinoujscie.
Bomu
hilo liitwalo Tallboy au ''tetemeko la ardhi'' lilidondoshwa wakati wa vita ya
pili ya dunia na kuizamisha meli ya Ujerumani Lützow.
Swinoujscie
ilikuwa sehemu ya Ujerumani na kuiita Swinemünde wakati wa ulipuaji.
Mtikisiko
wakati wa kulitegua bomu hilo ulisikika katika sehemu za mji na video
zinaonesha mlipuko mkubwa na maji mengi yakiruka angani.
Bomu
hilo lilikuwa na urefu wa mita 6 na uzito wa tani 5.4, karibu nusu ya bomu hilo
liliundwa na vilipuzi.
Lilikuwa limetua kwenye kina cha mita 12 na sehemu ya pua ya bomu hilo ilikua ikichungulia nje.
EmoticonEmoticon