Kidokezo
kimoja ambacho kinastahili kuzingatiwa na jinsia zote mbili kwa mujibu wa
wataalamu ni kwamba wanaume na wanawake wanashauriwa kwenda haja ndogo kabla na
baada ya kufanya tendo la ndoa.
"Kwenda
haja ndogo baada ya kufanya tendo la ndoa ni moja ya njia muhimu ya kujiepusha
na magonjwa yanayosababishwa na bakteria, " anasema Martínez.
"Kujisaidia
haja ndogo baada ya tendo la ndoa kunasaidia kusafisha kibofu cha mkojo, hali
ambayo inazuia bakteria kuathiri sehemu hiyo," anaeleza
"Pia
kwenda haja ndogo kabla ya tendo la ndoa ni muhimu, kwani wapenzi watakaribiana
bila kuwa na hofu ."
Briet
anaongeza kuwa mwenendo huo "ni mzuri kwani unaweza kuzuia magonjwa
yanayoathiri njia ya kupitisha mkojo kwa kiwango kikubwa hata kama sio magonjwa
mengine."
Wataalamu
wa saikolojia ya ngono wanapendekeza wapenzi kwenda haja ndogo "punde
baada ya kufanya tendo la ndoa" ili kujikinga na magonjwa na kupunguza
uwezekano wa kuambukizwa magonjwa.
Kulingana
na wataalamu hao wanawake wako katika hatari ya kupata maabukizi ya magonjwa
yanayoathiri njia ya kupitisha mkojo. Hivyo basi wanapendekeza wawe na mazoea
ya kwenda haja dakika 15 kabla ya kushiriki tendo la ndoa.
Utafiti
uliochapishwa katika jarida la matibabu la ustawi wa familia(2002) unasema kuwa
wanawake wenye afya ambao huenda haja dakika 15 kabla ya kujamiiana huenda
wakajiepusha na hatari ya kupata maambukizi wakilinganishwa na wenzao ambao
hawafanyi hivyo.
Mapendekezo makuu:
Osha sehemu
za siri kila siku kwa kutumia maji.
Piga mswaki.
Valia nguo
za ndani safi, zilizotengenezwa kutokana na pamba ni bora zaidi.
Muone
daktari angalau mara moja kwa mwaka ufanyiwe uchunguzi wa kimatibabu.
Kuwa na
mazoea ya kujichunguza endapo utaona mabadiliko yoyote katika sehemu za siri
muone dakatari.
Tumia
kondomu wakati wa tendo la ndoa.
Inapendekezwa usiwe na mazoea ya kunyoa nywele zote zinaoota katika sehemu za siri, kwasababu zinatumika kama kinga, bora kupunguza kidogo.
EmoticonEmoticon