Mamlaka ya
Marekani yameiidhinisha dawa aina ya remdesivir kuwatibu wagonjwa wa Covid-19
hospitalini.
Mamlaka
ya chakula na dawa nchini Marekani (FDA) imesema Veklury, ambalo ni jina la
dawa sokoni, imeweza kuwasaidia wagonjwa katika wastani wa siku tano wakati wa
majaribio.
"Veklury
ni dawa ya kwanza kuidhinishwa na mamlaka ya chakula na dawa kutibu ugonjwa wa
corona," FDA ilieleza kwenye taarifa yake.
Wiki
iliyopita Shirika la afya duniani (WHO) lilisema kuna ushahidi mdogo kuhusu
ufanisi wa dawa ya remdesivir kumponya mgonjwa wa Covid 19.
WHO
lilisema hii ni kutokana na utafiti wake, lakini mtengenezaji wa dawa hiyo
kampun ya Gilead alikataa matokeo ya jaribio lililofanywa.
Remdesivir
ilikuwa inaruhusiwa kutumika wakati wa dharura pekee nchini Marekani tangu
mwezi Mei.
Hivi
karibuni Rais Donald Trump alipatiwa dawa hiyo baada ya kupata maambukizi ya
virusi vya corona.
Katika
taarifa iliyotolewa na FDA , imesema dawa hiyo iliidhinishwa Alhamisi kwa ajili
ya matumizi ya watu wazima na wenye umri wa miaka 12 na zaidi ambao wana kilo
takribani 40, na wale ambao watakuwa wamelazwa kwa ajili ya kutibiwa corona.
"Leo
hii kuidhinishwa kwa dawa hiyo imeambatanishwa na takwimu za matokeo ya
majaribio kadhaa yaliofanyika kuthibitisha na kuona kuwa ni hatua kubwa muhimu
ya kisayansi imefikiwa katika kukabiliana na janga la virusi vya corona,"
alisema msimamizi wa FDA Stephen Hahn.
Mamlaka
hiyo imesema uamuzi huo uliungwa mkono na uchambuzi wa data kutoka kwa
majaribio matatu ambayo yilijumuisha wagonjwa waliolazwa kutokana na Covid 19
na wale ambao hawakuathirika sana na Covid-19.
Utafiti mmojawapo umeonesha kuwa ''wastani wa muda wa kupona Covid-19 kwa kutumia dawa ya Veklury ilikuwa siku 10 tofauti na nyingine za placebo kuwa siku 15".
EmoticonEmoticon