Ajali ya
ndege mbili za kijeshi aina ya helkopta za Afghanistan zimesababisha wanajeshi
kujeruhiwa huko kusini mwa jimbo la Helmand na wengine tisa kufariki.
Wote
waliofariki walikuwa ndani ya ndege hizo, maofisa wamesema.
Tukio
hilo limetokea mapema Jumatano katika kitongoji cha Nawa na ajali hiyo
ilisababishwa na tatizo la kiufundi.
Eneo
hilo limekuwa na mapigano hivi karibuni kati ya Taliban na jeshi la serikali ya
Afghanistan , wakiungwa mkono na wanajeshi wa angani kutoka Marekani.
Mapigano
hayo yamekuwa yakiendelea pembezoni mwa mji wa Lashkar Gah ambako kulikuwa
tayari kumedhibitiwa
Umoja wa mataifa unasema zaidi ya watu 35,000 wamelazimika kuhama makazi yao huko Helmand.
EmoticonEmoticon