Mmoja wa
wakosoaji wakubwa wa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema
kauli yake ya hivi karibuni kuhusu wapenzi wa jinsia moja ni maoni binafsi
ambayo hayastahili kuzingatiwa na Wakatoliki.
Kadinali
Raymond Burke anayeonekana kuwa mhafidhina katika Kanisa Katoliki, ametoa tamko
hilo siku chache baada ya Papa Francis kuonekana kuunga mkono wazo la
kutambuliwa kisheria kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.
Kadinali
Burke anasema pendekezo la Papa Francis la kutaka ndoa ya wapenzi wa jinsia
moja kutambuliwa kisheria halijawashangaza wengi lakini maneno aliyotumia ndio
yaliyowashangaza sana viongozi wa kidini na waumini wa Kanisa Katoliki.
Kadinali
huyo ametaja matamshi ya Papa kama maoni ya kibinafsi na kwamba Kanisa katoliki
na waumini wake hawatashurutishwa kutii msimamo wa kiongozi wa Kanisa hilo
kuhusu suala la wapenzi wa jinsia moja.
Pia
amesema viongozi wa kidini wa kanisa hilo wana jukumu la kutoa kile
alichokitaja kama maelezo ya kina kuhusu suala hilo.
Kadinali Burke amesema imani rasmi ya kanisa Katoliki la Roma ni kuwa ndoa ya wapenzi wa jinsia moja hairuhisiwi na kwamba matamshi hayo ya papa yamewahuzunisha waumini wengi akidai kuwa matamshi ya papa hayaambatani na mafundisho ya Kanisa hilo.
EmoticonEmoticon