Vatican imemkatalia waziri wa mambo ya
nje wa Marekani, Mike Pompeo kuonana na Papa Francis.
Kiongozi huyo wa juu wa Kanisa Katoliki
ameelezwa kuwa hawapokei wanasiasa wakati wa kipindi cha uchaguzi.
Hatua hiyo inaongeza hali ya mzozo wa
kidiplomasia baada ya kauli ya Bwana Pompeo kuhusu China na Kanisa Katoliki.
Vatican ilimshutumu Pompeo kuwa anajaribu
kutumia suala hilo kuvutia wapiga kura wa uchaguzi wa urais wa mwezi Novemba
nchini Marekani.
Katika makala ya mwanzoni mwa mwezi
Septemba, Bwana Pompeo alisema kanisa Katoliki linapoteza ''mamlaka yake ya
kinidhamu'' kwa kufanya makubaliano mapya na China kuhusu uteuzi wa maaskofu.
Donald Trump anapata uungwaji mkono
kutoka kwa mashirika ya kidini ya kihafidhina, pamoja na wapiga kura wa
Kikatoliki wa kihafidhina, ambao wengine wanadhani Papa Francis ni mtu mwenye
uhuru sana.
Makundi ya haki za binadamu yanasema kuwa Wakatoliki wengi nchini China wanateswa kwa kuahidi utii kwa Papa badala ya chama rasmi cha Wakatoliki nchini China.
EmoticonEmoticon