Rais mteule wa Marekani amesema
atawaomba raia wa Marekani kuvaa barakoa siku 100 za mwanzo za utawala wake ili
kupunguza maambukizi ya virusi vya corona. Katika mahojiano aliyoyafanya na Jake Tapper wa CNN, bwana
Biden alisema: "Siku ya kwanza nitakayoapishwa nitawaomba wananchi kuvaa
barakoa kwa siku 100 na sio milele.
"Na nadhani itaweza kusaidi kupunguza maambukizi kwa
kiasi kikubwa sana, kama chanjo na barakoa zitaweza kupunguza
maambukizi."
Wataalam wa katiba wanasema rais wa Marekani hana mamlaka ya
kutoa amri kwa watu kuvaa barakoa lakini bwana Biden alisema wakati wa
mahojiano hayo kuwa makamu wake wa rais Kamala Harris ataweka mfano wa namna ya
kufunika uso.
Mamlaka ya
rais yanahusisha kulinda mali za serikali ya Marekani, na bwana Biden aliiambia
CNN kuwa ana lengo la kutumia mamlaka hayo.
"Ninaenda kutoa agizo katika serikali ya shirikisho kuwa
wanapashwa kuvaa barakoa," alisema.
Aliongeza: "Katika upande wa usafirishaji,kila mtu
anapaswa kuvaa barakoa kwenye ndege na mabasi na usafiri wowote."
Ndege za Marekani , uwanja wa ndege na maeneo mengi ya umma tayari yanawataka abiria na wafanyakazi wake kuvaa barakoa. White House ya Trump imekataa kufuata agizo hilo kutoka kwa wataalamu wa afya.
Alizungumza huku Gavana wa California Gavin Newsom akitoa amri ya kukaa nyumbani kwa sehemu kubwa ya wakazi wa jimbo lake , akisema ana weka ''mapumziko ya dharura " huku wagonjwa wa virusi wakitishia kupita uwezo wa hospitali .
EmoticonEmoticon