Maafisa wa Marekani wamesema chanjo ya virusi vya corona iliyotengenezwa na kampuni mbili za Pfizer na BioNTech itaanza kutolewa kwa mara ya kwanza kesho Jumatatu siku kadhaa tangu matumizi yake yalipoidhinishwa.
Jenerali wa Jeshi la Marekani anayesimamia usambazaji wa chanjo
hiyo, Gus Perna, amesema dozi za kwanza zitasafirishwa leo Jumapili na hapo
kesho zoezi ya utoaji chanjo litaanza kwa asilimia 100.
Perna
amearifu kuwa ifikapo kesho vituo vya kutolea chanjo 145 vitakuwa vimepokea
shehena ya kwanza, huku vituo 425 vitapelekewa chanjo siku ya Jumanne na chanjo
hiyo itapokelewa pia kwenye vituo vingine 66 siku ya Jumatano.
Kampuni
inayotengeneza chanjo hiyo imesema inafanya kazi na washirika wengine kuanza
kusafirisha chanjo kwa kutumia magari ya mizigo kutoka kwenye maghala yake
yaliyoko kwenye majimbo Michigan na Wisconsin kwenda majimbo yote 50 ya
Marekani.
Chanjo hiyo ni lazima ihafidhiwe kwenye baridi ya nyuzi -70 C, hali inayoleta changamoto itakayotatuliwa kwa kutumia barafu na kontena maalum zilizotengenezwa kwa ajili ya kuhifadhi shehena yake.
EmoticonEmoticon