Serikali ya
Somalia imetangaza kusitisha uhusiano wake na Kenya ikidai kwamba serikali ya
Kenya inaingilia kati maswala yake ya ndani.
Nchi hiyo
jirani wa Kenya, imetangaza kuwafukuza wanadiplomasia wote wa Kenya na kuagiza
wanadiplomasia wake wote walio Nairobi kurudi Mogadishu ndani ya siku saba
kuanzia leo jumanne Desemba 15 2020.
Waziri wa
habari wa Somalia Osman Abukar Dubbe, amesema katika hotuba iliyopeperushwa
moja kwa moja na televisheni ya serikali ya Somalia Jumatatu jioni kwamba hatua
hiyo imechukuliwa kujibu uchokozi wa kisiasa wa kila mara unaofanywa na
serikali ya Kenya kinyume na uhuru wa Somalia.
Serikali ya Kenya haijajibu madai wala hatua hiyo ya Somalia.
CREDIT:Voa
EmoticonEmoticon