Israel
itafanya uchaguzi wake wa nne katika kipindi cha miaka miwili baada ya vyama
vikuu viwili katika serikali ya umoja kushindwa kuheshimu muda wa mwisho wa
kutatua mzozo juu ya bajeti ya taifa.
Wapigakura watarejea katika uchaguzi mwezi Machi, miezi 12 tu
baada ya awamu ya uchaguzi kufanyika.
Uchaguzi wa awali haukukamilika , na hivyo kusababisha
kuundwa kwa serikali nadra ya umoja.
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu, ambaye kesi ya madai ya
ufisadi inaendelea dhidi yake, ana matumaini ya kurejea madarakani kwa muhula
wa sita.
Alikana mashitaka ya uhalifu, ambayo aliyapuuzilia mbali
akiyataka kuwa yenye uchochezi wa kisiasa.
Jumanne usiku, bunge la Israeli-Knesset, lilivunjwa moja kwa
moja kulinga na sheria baada ya makataa ya mwisho kupita ya kuidhinishwa kwa
bajeti ya mwaka 2020.
Jaribio la saa 11 la kuepuka kuvunjwa kwa bunge lilishindwa baada ya muswada wa kurugusu kuongezwa kwa muda wa majadiliano zaidi kupingwa kwa kura, kinyume na ilivyo tarajiwa.
EmoticonEmoticon