Wataalam wa
usalama wa Nigeria wanatia shaka madai ya maafisa kwamba uhasama kati ya
wakulima na wafugaji wa ng'ombe ulisababisha wimbi la utekaji nyara hivi
karibuni katika jimbo la Katsina lililopo kaskazini magharibi mwa nchi.
Wanafunzi wavulana zaidi ya 300 walitekwa nyara mapema mwezi huu lakini baadaye
wakaachiliwa huru.
Mamlaka huko
Katsina mwanzoni ililaumu utekaji nyara wa wavulana wa shule 344 kwa magenge ya
majambazi ambao wamewateka nyara baadhi ya watu kwa ajili ya kulipwa fidia
katika jimbo la kaskazini magharibi mwa Nigeria.
Halafu
maafisa walibadilisha usemi wao , wakidai utekaji huo unahusiana na mzozo kati
ya wafugaji ng'ombe na wakulima juu ya matumizi ya ardhi.
Lakini
kamishna mstaafu wa polisi na mchambuzi wa usalama Lawrence Alobi hakubaliani
na wazo hilo kwamba wafugaji walifanya shambulizi hilo.
"Wafugaji
hawana shida yoyote na wakuu wa shule au wanafunzi. Shida yao iko kwa wakulima,
mahali ambako wanaweza kulisha ng'ombe wao. Kwa hivyo, sijui uhusiano kati ya
utekaji nyara wa wanafunzi hao na mivutano na wakulima.” alisema Alobi.
Kikundi cha
wanamgambo wa Kiislam Boko Haram kilidai kuhusika na utekaji nyara wa wavulana
hao wa shule na kutoa picha ya video inayoonyesha baadhi ya wavulana waliotekwa
kabla ya kuachiliwa huru.
Madai hayo, ikiwa yatathibitishwa, yangeashiria mabadiliko kwa kundi hilo, ambalo hadi sasa limekuwa likifanya kazi hasa katika upande wa kaskazini mashariki mwa nchi.
EmoticonEmoticon