Dustin
Higgs, mfungwa aliyekuwa amehukumiwa kifo katika gereza la Indiana, amenyongwa
katika utekelezaji wa mwisho wa adhabu hiyo chini ya utawala wa wa Rais wa
Marekani Donald Trump siku chache kabla aondoke madarakani.
Higgs alipewa hukumu hiyo baada ya kuwaua wanawake watatu
waliokuwa wamejifichwa katika mbuga ya wanyama mwaka 1996, lakini hadi kifo
chake alikana kutoa amri ya mauaji hayo.
Alifariki baada ya kudungwa sindano ya sumu saa saba na
dakika ishirini na tatu majira ya mji huo sawa na (06:23 GMT) siku ya Jumamosi.
Mauaji yake ni 13 kutekelezwa tangu mwezi Julai baada ya
Marekani kusitisha utekelezaji wa hukumu ya kifo miaka 17 iliyopita.
Hatua hiyo inajiri siku chache kabla ya Rais Mteule Joe Biden, ambaye anapinga adhabu ya kifo, kuapishwa.
EmoticonEmoticon