Baraza la Seneti la Bunge la
Marekani limepiga kura na kumuidhinisha kwa wingi mkubwa mwanauchumi
anayeheshimika Janet Yellen kuwa Waziri wa Fedha wa Taifa hilo.
Wajumbe wa Seneti wamemuidhinisha Yellen kwa kura 84 za ndio
dhidi ya 15 za hapana na kumfanya kuwa Mwanamke wa kwanza kuongoza Wizara hiyo
tangu ilipoanzishwa zaidi ya miaka 200 iliyopita.
Yellen anatajwa kuwa miongoni mwa wachumi wenye tajriba kubwa
baada ya hapo kabla kufanya kazi kama Gavana wa Benki Kuu ya Marekani na Mjumbe
wa Baraza la Washauri wa Uchumi wa Ikulu ya White House.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon