China
imeipiku Marekani kama eneo linalolengwa na uwekezaji wa moja kwa moja wa
kigeni kulingana na takwimu za UN zilizotolewa siku ya Jumapili.
Nusu ya uwekezaji mpya nchini Marekani kutoka katika
makampuni ya kigeni ulishuka mwaka uliopita hatua iliosababisha taifa hilo
kupoteza nafasi yake ya kwanza.
Kwa upande mwingine, takwimu hizo zinaonyesha uwekezaji wa
moja kwa moja katika kampuni za Wachina uliongezeka kwa asilimia 4 , na
kulifanya taifa hilo kuchukua nafasi ya kwanza duniani.
Kupanda kwa China kunaonesha ushawishi wake katika sekta ya
kiuchumi duniani.
China ilijipatia kipato cha $163bn (£119bn) mwaka uliopita , ikilinganishwa na $134bn zilizoingia Marekani, Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Biashara na Maenedeleo (UNCTAD) ulisema katika ripoti yake.
EmoticonEmoticon