Utawala wa Rais Joe Biden umesitisha kwa muda uuzaji wa silaha kwa mataifa ya Ghuba.
Hatua hii inazuia mabilioni ya
dola kwa mauzo ya silaha na kubadili maamuzi ya mwisho ya rais aliyeondoka
madarakani Donald Trump. Wizara ya mambo ya nje imesema itaikagua mikataba iliyotiwa saini na
Trump kabla ya kuibatilisha au kuendelea nayo.
Utawala wa Biden Jumatano umetangaza kuwa utazuilia kwa muda mabilioni ya dola katika mauzo ya silaha kwa Umoja wa Falme za Kiarabu na Saudi Arabia.
Waziri wa mambo
ya Nje, Antony Blinken ameitaja hatua hiyo "kama ya kawaida
kiutawala" akibainisha kuwa ilikuwa kawaida kwa utawala unaoingia
madarakani kuipitia mikataba mikubwa ya silaha iliyoanzishwa na utawala
uliomaliza muda wake.
Wizara hiyo
imesema kusitisha kwa muda kutaruhusu utawala wa Biden kuhakikisha mauzo ya
silaha za Marekani yanatimiza malengo ya kimkakati ya kujenga washirika wenye
usalama, ushirikiano na uwezo.
Blinken katika siku yake ya kwanza ofisini Jumatano, amesema utawala mpya umeanzisha uchunguzi kamili wa uhusiano kati ya Marekani na Urusi pia inachunguza maelezo ya mkataba wa amani wa Marekani na Taliban uliosainiwa karibu mwaka mmoja uliopita.
EmoticonEmoticon