Iran
inapanga kuanza tena kurutubisha madini yake ya uranium yaani urani kwa asilimia
20, hayo ni kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kudhibiti matumizi ya
nishati ya atomiki (IAEA), hatua ambayo hadi kufikia sasa itakuwa ni ukiukaji
mkubwa wa makubaliano ya kimataifa ya nyuklia.
Hiyo inamaanisha kwamba Iran itakuwa na mapungufu ya asilimia
90 ya kiwango kinachohitajika kutengeneza bomu la nyuklia.
Lakini kulingana na makubaliano ya mwaka 2015, Iran
ilihitajika kuimarisha madini yake ya uraniaum kwa kiwango cha chini ya
asilimia 4.
Iran ilianza kukiuka makubaliano hayo baada ya rais Trump
kuindoa Marekani kwenye makubaliano yaliyokuwa yamefikiwa na kuiwekea tena nchi
hiyo vikwazo. ambavyo vimeyumba pakubwa uchumi wa nchi hiyo.
Hata hivyo, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ufaranza na Uchina zote zina matumaini kuwa uhusiano wa pande hizo mbili unafursa ya kuimarika tena.
EmoticonEmoticon