Serikali ya Zimbabwe imesitisha
shughuli za maisha ya kawaida kote Nchini humo kufuatia kuongezeka kwa
maambukizi ya Covid-19, hatua inayowaweka katika hali ngumu Raia wake
wanaotegemea ajira ya sekta isiyo rasmi itachukua siku 30.
Waziri wa afya Constantino Chiwenga amesema kumekuwa na
ongezeko kubwa katika msimu huu wa sherehe ambalo liliongeza marudufu idadi ya
maambukizi yaliyorekodiwa katika mwaka mzima.
Ni huduma muhimu pekee kama vile hospitali, maduka ya dawa na
maduka ya jumla yatakayoendelea kufanya kazi kwa siku 30 zijazo, hali
inayoongeza mbinyo kwa familia ambazo tayari zinasumbuliwa na umaskini huku
taifa hilo likikabiliwa na mgogoro mkali wa kiuchumi, mfumuko wa bei na kiwango
cha juu cha ukosefu wa ajira.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon