Wanamgambo
wa Al-Shabab nchini Somalia wamehusika katika makabiliano ya polisi na vikosi
vya usalama katika hoteli moja iliyopo mji mkuu wa Mogadishu.
Kundi la Al-Shabab limekiri kutekeleza shambulizi hilo katika
hoteli ya Afrik ambalo lilianza na bomu lililokuwa limetegwa kweye gari
Jumapili mchana.
Hadi kufikia sasa, haijafahamika ni watu wangapi
waliojeruhiwa lakini shirika la habari la AFP limeripoti kuwa karibu watu
watatu wamefariki dunia.
Kundi hilo ambalo linahusishwa na kundi la wanamgambo la
Al-Qaeda, mara nyingi hutekeleza mashambulizi dhidi ya serikali.
Inasemekana kuwa gari moja liligonga eneo la mbele la hoteli
hiyo na kulipuka kabla ya mshambuliaji aliyekuwa amejihami kwa silaha kuvamia
jengo la hoteli, kulingana na maafisa na wengine walioshuhudia shambulizi hilo.
"Mlipuko
huo ulifanya hoteli hiyo ikaanza kutetemeka wakati tukiwa ndani tunaendelea na
mzungumzo. tulishutuka, tusijue la kufanya," aliyeshuhudia Ahmed Nur
amenukuliwa na shirika la habari la Reuters.
Maafisa waandamizi wa usalama Mohamed Dahir ameliambia shirika la AFP kuwa raia wawili na afisa mmoja wa usalama wamethibitishwa kufariki dunia, "lakini idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka."
EmoticonEmoticon