Barcelona
imesema kuwa itachukua "hatua za kisheria" dhidi ya gazeti la
Uhispania la El Mundo baada ya kuchapisha maelezo kuhusu mkataba wa
mshambuliaji, Lionel Messi wa pauni milioni 492.
Barcelona ilikanusha kuhusika kwa namna yoyote ile katika
uchapishaji wa taarifa hizo.
Kwa mujibu wa El Mundo, mkataba wa Messi wa miaka minne
ulikuwa wa thamani ya takriban euro 555,237,619 hadi Juni 30, 2021.
Hii inamaanisha kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 33,
atakuwa anapokea pauni milioni 123 kwa msimu.
Barcelona
imesema katika taarifa iliyotoa kuwa "inasikitishwa na uchapishaji wa
maelezo hayo". Na kuongeza kuwa: "FC Barcelona haihusiki kwa namna
yoyote ile katika uchapishaji wa taarifa hiyo na itachukua hatua stahiki za
kisheria dhidi ya gazeti la El Mundo, kwa uharibifu wowote ule ambao huenda
umetokea kwasababu ya taarifa hiyo.
"FC Barcelona imeonesha kumuunga mkono Lionel Messi,
hasa katika jaribio lolote la kumdhalilisha na kuharibu uhusiano wake katika
klabu hiyo ambako amefanyakazi na kuwa mchezaji bora duniani na katika historia
ya soka."
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina Messi alijiunga na
Barcelona akiwa na umri wa miaka 13 lakini akatuma ombi la kutaka aruhusiwe
kuhamia kwingineko mnamo mwezi Agosti.
Bado haijafahamiki ikiwa atabaki katika klabu hiyo wakati mkataba wake utakapomalizika.
EmoticonEmoticon