Siku kadhaa
baada ya mkuu wa michezo ya Olimpiki nchini Japani kulazimishwa kujiuzulu
kwasababu ya maneno yake ya kudhalilisha wanawake, chama chake kimeamua kualika
wanawake kuhudhuria mikutano muhimu - mradi tu wasiseme neno.
Chama cha Liberal Democratic (LDP) kilipendekeza wabunge
wanawake washuhudie bodi ambayo ina wanaume tu namna wanavyoendesha mkutano
wao.
Hawaruhusiwi kuzungumza wakati wa mkutano - lakini wanaweza
kutoa maoni yao baadaye.
Wanawake nchini Japani kwa kipindi kirefu wamekuwa wakijitenga
na ushiriki wa kisiasa na kiuchumi.
Nchi hiyo
imeorodheshwa kuwa ya 121 kati ya nchi 153 kulingana na kipimo cha Jukwaa la
Kiuchumi Duniani mwaka 2020 cha tofauti la kijinsia Duniani.
Wanawake wawili sasa hivi ndio wanaoshiriki katika bodi ya
watu 12 ya chama cha LDP ambacho kimekuwa madarakani karibu kila wakati tangu
mwaka 1955.
Toshihiro Nikai, 82, katibu mkuu wa chama cha LDP,
amezungumza na wanahabari Jumanne kwamba anataka kukaribisha wanawake katika
mkutano huo.
Alisema anafahamu ukosoaji unaoendelea dhidi ya wanaume
kutawala bodi ya chama hicho na ilikuwa muhimu kwa wanachama wa kike wa chama
hicho kufuatilia mchakato wa maamuzi unavyoendeshwa, alinukuliwa na shirika la
habari la Reuters
"Ni muhimu kuelewa majadiliano yanavyoendelea. Kutazama
na kufuatilia," alisema.
Chombo cha habari nchini Japani kimesema wanawake watano
huenda wakaruhusiwa kuketi na kufuatilia mkutano wa bodi inayofanya maamuzi
lakini hawataruhusiwa kuzungumza. Wanaweza kuwasilisha maoni yao baadaye kwa
Sekretarieti.
Sasa hivi wanasiasa 46 kati ya 465 nchini Japani ndio waakilishi wa wanawake - hiyo ikiwa ni takriban asilimia 10 ikilinganishwa na asilimia 25 kote duniani.
EmoticonEmoticon