Uchina sasa
ndio mshirika mkubwa zaidi wa biashara wa Muungano wa Ulaya, ikiipiku Marekani
katika mwaka 2020.
Uchina imeonesha kuwa na shughuli kubwa za biashara, huku
biashara na washirika wakuu wa Muungano wa Ulaya ikipungua kutokana na janga la
Covid-19.
Biashara baina ya Uchina na EU ilikuwa ya thamani ya dola
bilioni 709b (€586bn, £511bn) mwaka jana, huku Marekani ikifanya biashara ya
thamani ya dola bilioni 671 ya mauzo na uajizaji wa bidhaa kutoka Marekani.
Ingawa uchumi wa Uchina uliyumba katika kipindi cha robo ya
mwaka jana kutokana nan a janga la corona, uchumi wake uliinuka baadae mwaka
huo na kuchochea uhitaji wa bidhaa za Uchina kutoka Muungano wa Ulaya.
China lilikuwa ndilo taifa pekee lemnye uchumi mkubwa duniani kushuhudia ukuaji wa uchumi katika mwaka 2020, na hivyo kupata soko la magari ya Ulaya na bidhaa za anasa.
EmoticonEmoticon