Mwanamfalme
Harry na mkewe Meghan hawatarejelea shughuli za kifalme, kulingana na Makao ya
Kifalme ya Buckingham.
Malkia amethibitisha kwamba Mwanamfalme Harry na mkewe Meghan
"hawataendelea na majukumu yao ya kuhudumia umma".
Taarifa kutoka makao ya Kifalme imeongeza kuwa Mwanamfalme
Harry na mkewe Meghan "bado wanasalia kuwa wanafamilia wanaopendwa".
Wawili hao wamesema "utoaji huduma ni kokote" na
wamejitolea kuendelea kusaidia mashirika wanayowakilisha.
Mwanamfalme Harry na mkewe Meghan Januari iliyopita walisema kwamba watajiondoa kama "waandamizi" katika familia ya Kifalme na kuanza kufanya kazi ili waweze kujitegemea.
EmoticonEmoticon