Waziri mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern ametangaza vizuizi vya kufunga shughuli kwa siku tatu katika mji mkubwa wa Auckland baada ya kugundulika visa vitatu vya virusi vya corona.
Hata hivyo visa hivyo visa hivyo
bado havijatambuliwa huku baadhi ya mataifa ya Ulaya yakifunga mipaka ili
kuzuia kusambaa kwa virusi vinavyobadilika vya coronaWanafunzi wawili Hong Kong
waambukizwa kirusi kipya. Hali bado ni tete kufuatia kusambaa zaidi kwa virusi
hivyo vipya.
Baada ya kikao cha dharura na baraza la mawaziri waziri mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern alisema wameamua kuchukua mwelekeo wa tahadhari hadi pale watakapokuwa na taarifa zaidi kuhusu mlipuko huo.
Visa hivyo vitatu vinahusisha mtu na mke
wake pamoja na binti yao na ni vya kwanza kugundulika ndani ya taifa hilo tangu
Januari 24.
Vizuizi vya
kufunga shughuli vinarejeshwa tena kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miezi
sita nchini New Zealand na kuonekana pigo dhidi ya mafanikio makubwa
ya kulidhibiti janga hilo nchini humo.
Alisema, "Kitu kikubwa ninachowaomba watu wa Auckland ni kubaki nyumbani ili kuzuia hatari ya kusambaa. Watu wanatakiwa kufanya kazi kutokea nyumbani, labda tu kama haiwezekani. Kama utatoka nje, tafadhali kaa mbali kwa umbali wa mita mbili ama uko kwenye maeneo yenye usimamizi ambayo unajua kuna watu wengine, basi ni mita moja."
EmoticonEmoticon